ASKOFU MUSHI KUZIKWA JUMATANO
MAZISHI ya marehemu Askofu Veratus Gabriel Mushi wa
kanisa katoliki jimbo la zanzibar aliyweuawa kwa kupigwa risasi jana
asubuhi yanatarajia kufanyika Jumatano katika makaburi ya Kitope mkoa wa Kaskazini Unguja.
Akizungungumza na waandishi wa
habari ofisini kwake Shangani mjini Zanzibar, Askofu Mkuu wa Kanisa hilo
jimbo la Zanzibar Agostino Shao alisema kanisa lake limepokea kwa
mshtuko tukio hilo na kwamba linaendelea na maandalizi ya mazishi
yanayotarajiwa kufanyika katika makaburi ya viongozi wa kanisa hilo
katika kijiji cha Kitope, wilaya ya Kaskazini 'B', Unguja.
Alisema
kanisa lake linafanya mawasiliano na ndugu wa marehemu ili kujua ni
watu gani wataotaka kuhudhuria katika mazishi hayo pamoja na wageni.
"Tunachokifanya
toka jana baada ya kukabidhiwa mwili wa marehemu majira ya saa kumi
jioni ni kuratibu juu ya namna ya mazishi yatakavyokuwa pamoja na wageni
tunaotarajia kuwapokea katika mazishi hayo", alisema Askofu Shao.
Pamoja
na kuelezwa kuridhishwa kwake na hatua zilizochukuliwa na jeshi la
polisi toka kutokea kwa tukio hilo, Askofu Shao alisema ipo haja kwa
jeshi hilo kuhakikisha linawajibika ipasavyo ili kukomesha vitendo vya
uhalifu si tu kwa viongozi wa dini na maeneo yao ya ibada bali pia kwa
raia wote.
Akionesha kutoridhika na kutofanyiwa kazi
kwa taarifa za kutokea kwa matukio mbali mbali dhidi ya kanisa na
viongozi wake, askofu huyo alisema kuna haja maalum kwa Rais kufanya
marekebisho ya uongozi wa jeshi hilo kwa upande wa Zanzibar ili lifanye
kazi kwa kuzingatia sheria na kufanya juhudi katika kuzuia uhalifu kabla
ya kutokea.
"Kuna taarifa nyingi tumekuwa tukitoa kwa
jeshi la polisi lakni taarifa hizi zimekuwa hazifanyiwi kazi kikamilifu
na kuwa ndio chanzo cha matukio mengi ya kihalifu ndani ya nchi",
alisema Askofu Shao.
Monday, February 18, 2013
SMZ YATOA TAMKO
SERIKALI ITWASAKA WALIOMUUA ASKOFU MUSHI
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wananchi wa imani zote kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kuviwezesha kufanya uchunguzi wa kifo cha Askofu Varistus Gabriel Mushi kilichotokea jana asubuhi.
Akitoa taarifa ya serikali, Waziri wa nchi Afisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Muhammed Aboud Muhammed ofisini kwake Vuga, alisema serikali italiwezehsa jeshi la polisi na vyombo vyengine ulinzi na usalama ili kubaini chanzo cha matukio hayo yanayoonekana kushamiri siku hadi siku.
Abuod alisema katika wakati huu wa majonzi wananchi na waumini wa dini zote wanapaswa kutulia na kuviacha vyombo hivyo vifanye kazi zao kwa utaalamu na mafunzo yao.
"Serikali haiwezi kuacha matukio kama haya yaendelee kwani yanaibua hofu kwa jamii na kuathiri jina la nchi yetu na uchumi wetu kwa ujumla", alisema Aboud.
Aliongeza kuwa serikali ya Zanzibar inaunga mkono tamko lililotolewa na serikali ya muungano linalovitaka vyombo vya usalama vya ndani na nje ya nchi ili kubaini chanzo cha matukio hayo na kama kuna watu au kundi lolote linalofadhili matukio hayo.
Kuhusu suala la uwezekano wa kuzagaa kwa silaha, Aboud alisema hali hiyo inatokana na mazingira ya Zanzibar yanayowezesha kuwepo kwa bandari zisizo rasmi (bubu) jambo ambalo serikali inalifanyia kazi na kuwataka wananchi kutoa taarifa juu ya watu wanaowatilia shaka kuhusika na vitendo vya uhalifu.
Aidha aliwataka viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani , utulivu na kuvumiliana miongoni mwa waumini wao ili kuiepusha nchi na matatizo ya kijamii na kiuchumi.
"Kwa miaka mingi watu wa dini tofauti wamekuwa wakiishi pamoja kwa mafahamiano na mshikamano hivyo bado kila mmoja wetu anapaswa kutimiza wajibu wake ili kuendeleza mshikamano uliodumu kwa muda mrefu", aliongeza Aboud.
Askofu Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi tatu kichwani asubuhi ya Jumapili wakati akienda kuendesha misa ya Jumapili katika kanisa la mtakatifu Theressa liliopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar ambalo ni sehemu ya kanisa Katholiki jimbo kuu la Zanzibar.
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wananchi wa imani zote kutoa ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kuviwezesha kufanya uchunguzi wa kifo cha Askofu Varistus Gabriel Mushi kilichotokea jana asubuhi.
Akitoa taarifa ya serikali, Waziri wa nchi Afisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Muhammed Aboud Muhammed ofisini kwake Vuga, alisema serikali italiwezehsa jeshi la polisi na vyombo vyengine ulinzi na usalama ili kubaini chanzo cha matukio hayo yanayoonekana kushamiri siku hadi siku.
Abuod alisema katika wakati huu wa majonzi wananchi na waumini wa dini zote wanapaswa kutulia na kuviacha vyombo hivyo vifanye kazi zao kwa utaalamu na mafunzo yao.
"Serikali haiwezi kuacha matukio kama haya yaendelee kwani yanaibua hofu kwa jamii na kuathiri jina la nchi yetu na uchumi wetu kwa ujumla", alisema Aboud.
Aliongeza kuwa serikali ya Zanzibar inaunga mkono tamko lililotolewa na serikali ya muungano linalovitaka vyombo vya usalama vya ndani na nje ya nchi ili kubaini chanzo cha matukio hayo na kama kuna watu au kundi lolote linalofadhili matukio hayo.
Kuhusu suala la uwezekano wa kuzagaa kwa silaha, Aboud alisema hali hiyo inatokana na mazingira ya Zanzibar yanayowezesha kuwepo kwa bandari zisizo rasmi (bubu) jambo ambalo serikali inalifanyia kazi na kuwataka wananchi kutoa taarifa juu ya watu wanaowatilia shaka kuhusika na vitendo vya uhalifu.
Aidha aliwataka viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani , utulivu na kuvumiliana miongoni mwa waumini wao ili kuiepusha nchi na matatizo ya kijamii na kiuchumi.
"Kwa miaka mingi watu wa dini tofauti wamekuwa wakiishi pamoja kwa mafahamiano na mshikamano hivyo bado kila mmoja wetu anapaswa kutimiza wajibu wake ili kuendeleza mshikamano uliodumu kwa muda mrefu", aliongeza Aboud.
Askofu Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi tatu kichwani asubuhi ya Jumapili wakati akienda kuendesha misa ya Jumapili katika kanisa la mtakatifu Theressa liliopo Beit el Ras nje kidogo ya mji wa Zanzibar ambalo ni sehemu ya kanisa Katholiki jimbo kuu la Zanzibar.
Monday, January 28, 2013
KUMRADHI
Wandugu wapendwa, poleni kwa kutopokea habari na matukio mapya kwa muda mrefu sasa.
Hii ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu na kwamba najua mlivyosumbuka au kukosa huduma hii ya habari kwa muda wote.
Natanguliza shukurani kwa uvumilivu wenu na kuwaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Nategemea kuwa tutaendelea kuwa pamoja.
karibuni sana.
Hii ilitokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wangu na kwamba najua mlivyosumbuka au kukosa huduma hii ya habari kwa muda wote.
Natanguliza shukurani kwa uvumilivu wenu na kuwaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza.
Nategemea kuwa tutaendelea kuwa pamoja.
karibuni sana.
Monday, November 26, 2012
AFUTA HATI YA UMILIKI WA ARDHI
BALOZI SEIF ASITISHA UMILIKI WA ARDHI
- ATAKA MASLAHI YA WANYONGE YAZINGATIWE
- ATAKA WANANCHI, MAMLAKA KUHESHIMU SHERIA
Hatua hiyo imefikiwa kufuatia mgongano unaoendelea kujitokeza kati yake na wanakijiji
wa eneo hilo ambao unaashiria uvunjifu wa amani
baina ya mmiliki huyo na wanakijiji hao.
Aidha hatua hiyo pia inauzuia uongozi wa kituo cha kujiendeleza kielimu katika shehia hiyo kufanya shuguli
yoyote ya ujenzi kwa kile kilichogundulika kuwa umiliki wa eneo hilo hauko kihalali katika
vyombo vinavyosimamia masuala ya Ardhi.
Zuio hilo limetolewa hivi karibuni na Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofanya
ziara fupi katika eneo hilo baada ya malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wanaotumia maeneo hayo hao dhidi ya watu wanaodaiwa kumilikishwa mashamba hayo ambayo yalikuwa yakitumiwa na wizara ya kilimo.
Naibu katibu mkuu wa Wizara Kilimo na
Maliasili Juma Ali Juma alimthibitishia Makamu wa Pili wa Rais kwamba mmoja ya watu wanaodai kumiliki eneo hilo Kassim Hassan hakuwa na nyaraka halali za eneo hilo
ambalo ni lilikuwa ni milki ya Wizara ya Kilimo walilopewa baada ya mapinduzi ya ya Zanzibar ya 1964.
Juma alisema kutokana na maombi
na umuhimu wa ardhi kwa mahitaji ya jamii, serikali imeiagiza wizara hiyo
kupima eneo hilo ili baadae ligaiwe kwa wananchi kwa
lengo la kuendeleza mahitaji ya kilimo na ujenzi kazi ambayo alisema kuwa imeshakamika.
Malalamiko ya wanachi yalikwenda sambamba
na ule mzozo unaofukuta kati ya wakulima waliokuwa wakiendeleza shughuli za Kilimo
katika shamba la Bwana Abeid Said wakidai kwamba mmiliki huyo alikuwa akionyesha
dalili mbali mbali za kuhatarisha maisha ya mifugo
yao pamoja na vipando vyao.
Akitoa ufafanuzi wa kadhia hiyo
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliiagiza wizara ya kilimo kumtafutia shamba jengine Bwana Abei Said Shankar ili kuepuka shari.
“Nakuagizeni Wizara ya Kilimo
mhakikishe kuwa mnampatia eneo la kujenga nyumba mwananchi huyu masikini wa Mungu, mnampimia eneo la ujenzi Bwana Kassim kwa ajili ya kituo chao
waweze kumiliki kihalali pamoja na kumpatia shamba jengine bwana Abeid" aliagiza balozi Iddi na kuongeza kuwa hatua
hii itaondoa mvutano bila ya
migongano miongoni mwa jamii.
“Kama mtu anashindwa kuishi na jamii
inayomzunguka katika maeneo ya umiliki wa serikali mtu huyo inafaa aondoshwe na
mamlaka zinazosimamia umiliki huo wa Serikali ili kuepuka shari”. Alisisitiza
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar.
Aidha Balozi Seif aliiasa jamii kuheshimu sheria na taratibu zilizowekwa ili kuepuka mizozo
isiyokuwa na lazima na kutahadharisha kwamba ardhi itaendelea kuwa
mali ya serikali na haitasita kuitumia kwa maslahi ya umma.
Eneo hilo la ekari sita lililopo
katika kijiji cha Selemu, wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja kilichojaaliwa utajiri wa ardhi yenye rutba lililomilikishwa kwa wizara ya kilimo na mali asili Zanzibar tokea mwaka
1964.
CHANZO: OMPR
CHANZO: OMPR
Tuesday, November 6, 2012
MAHAFALI YA PILI FUONI
"TUSHIRIKIANE KUSAIDIA SEKTA YA ELIMU KWA MAENDELEO YA TAIFA" - BAUCHA
Wadau wa elimu nchini wametakiwa
kutoa mashirikiano kwa walimu ili kuinua kiwango cha ufaulu wa wanafunzi na
ubora wa elimu inayotolewa katika skuli za serikali na binafsi
nchini.
Akizungumza katika mahafali ya pili
ya wanafunzi wa skuli ya Fuoni Sekondari waliomaliza kidatu cha nne Mkurugenzi
wa biashara wa kampuni ya Zantel Moh’d Khamis Baucha alisema mashirikiano kati
ya pande hizo ndio njia pekee itakayoongeza kiwango cha kufaulu na kuleta
ufanisi kwa jamii nzima.
Alisema kuwa katika zama za sayansi
na teknolojia ni lazima kuwepo na njia mbadala zitakaziowezesha wanafunzi
kunufaika na elimu wanayoipata wakiwa skuli kama njia mojawapo ya kujikomboa na
umasikini na kujitegemea pindi wanapomaliza masomo.
“Zama zimebadilika sana, ipo haja kwa
wanafunzi, walimu, wazazi na wadau wengine kushirikiana na kuhakikisha
tunazingatia katika upatikanaji wa elimu bora na sio bora elimu tu”,
alisema.
Aidha aliwaasa wahitimu hao
kuhakikisha wanayatumia vyema mafunzo waliyoyapata wakati wanasubiri matokeo na
kuwa raia wema huku wakiwasaidia wanafunzi wanaoendelea situu kujua kusoma bali
pia kufahamu wanachosomeshwa.
“Wakati mkiondoka skuli ni vyema
mkayatumia masomo mliyoyapata na kuwasaidia wenzenu waliobaki kujua kusoma,
kufahamu wanachosomeshwa, na kuhesabu kama njia ya kujijengea uwezo wenu na wao
katika kufikiri na kupambanuua mambo,….. mkifikia hatua hiyo mtakuwa mmeelimika
kikamilifu”, aliongeza Meneja huyo.
Aidha aliahdi kuwa kampuni yake
italishughulikia tatizo la ukosefu wa vifaa vya maabara na kompyuta
linaloikabili skuli hiyo na kuwataka wadau wengine kujitokeza kusaidiaskuli hiyo
hususan uchakavu wa majengo ili kupata mazingira mazuri ya kujifunzia jambo
ambalo amedai lina mchango mkubwa katika upatikanaji wa elimu bora.
“Nimesikia kilio chenu, kwa kuanzia
nimekuja na ‘modem’ za ‘internet’ kwa ajili ya mtandao na nitakaa na wenzangu
katika kampuni kuangalia ni namna gani tunaweza kusaidia hasa masuala ya vifaa
vya maabara na kompyuta ili kuendana na wakati uliopo”, alisema Meneja
Baucha.
Akisoma risala ya walimu na
wanafunzi wa skuli hiyo, Mwalimu Sudi Mchenga alizitaja changamoto
za uhaba wa walimu hasa katika masomo ya sayansi, uchakavu wa majengo, uhaba wa
samani, vifaa vya maabara na kompyuta kuwa ni miongoni mwa mambo yanayokwaza
malengo yao ya kufaulisha, wanafunzi wengi zaidi kila mwaka.
“Pamoja na kupiga hatua za mafanikio
mwaka hadi mwaka, bado uchakavu wa majengo, samani na nyenzo nyengine za
kujifunzia na kufundishia zimekuwa ni matatizo yanayotukwaza kufikia malengo
yetu, hivyo tunawaomba wadau wote kutusaidia ili tutimize wajibu wetu
kikamilifu”, alisema Maalim Mchenga.
Mapema akimkaribisha mgeni rasmi
Kaimu Mkurugenzi wa idara ya elimu sekondari Zanzibar, Maalim Ali
Hamdani aliwataka wanafunzi wanaofaulu kuendelea na elimu ya juu nchini kufanya
maombi mapema katika bodi ya mikopo ya elimu ya juu ili kuepusha malalamiko ya
kunyimwa mikopo.
“Idadi ya wanafunzi wanaohitaji
mikopo imekuwa ikiongezeka kila mwaka hivyo basi wale watakaobahatika kuendelea
na masomo hasa ya elimu ya juu ni vyema wakafanya maombi mapema kabla bajeti
haijapitishwa ili kuweza kutoa mikopo kwa wanafunzi wengi zaidi”, alisema afisa
huyo akijibu ombi la kupatiwa mikopo kwa walimu wanaokwenda kusoma.
Aidha aliwataka walimu wanaopata
nafasi ya kwenda kusoma kurudi maskulini mwao ili kupunguza uhaba wa walimu
ambao amedai unachangiwa na baadhi yao kutorudi katika vituo vyao wanapomaliza
masomo na wengine kubadilisha kada kwa kisingizio cha maslahi duni jambo ambalo
alisema linachangia kupunguza idadi ya walimu.
Skuli ya Fuoni ni miongoni mwa skuli
kongwe zilizopo Zanzibar iliyoanzishwa mwaka 1952 ikitoa elimu ya awali ,msingi
ha kati kabla ya kubadilishwa kuwa ya sekondari, katika mahafali hayo
wanafunzi 129 wanaume 58 na wanawake 71 walikabidhiwa vyeti vya
kumalizia masomo idadi ambayo ni ziada ya wanafunzi 16 ya wanafunzi 113
waliomaliza mwaka jana ambapo kati yao wanafunzi 11, wanawake 7 na
wanaume 4 walifaulu na kuendelea na kidato cha tano katika skuli mbali
mbali.
SORAGA AMWAGIWA TINDIKALI
Monday, October 29, 2012
ZIARA YA MAKAMO WA 2 WA RAIS SMZ
NAKAGUA:
Mnamo oktoba 28, 2012 Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alifanya ziara ya siku moja kwa ajili ya kukagua miradi ya maendeleo iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi na kufadhiliwa na serikali au washirika wa maendeleo.
Ziara hiyo ilihusisha vijiji vya Bweleo, Fumba na Bwefum viliopo wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja. Haya ni baadhi ya matukio katika ziara hiyo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiangalia majengo
ya skuli ya Bwefum iliyoko Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini Magharibi ambayo Mapaa yake yako katika hali ya uchakavu akiwa na
Mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo Kesi Mwinyi Shomari pamoja na baadhi ya wanafunzi wa darasa la kwanza wa skuli hiyo.
Mwalimu mkuu wa skuli ya Bwefum, Kesi Mwinyi Shomari (wa kwanza kushoto aliyevaa kofia) akimuongoza Makamo wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kukagua majengo na eneo la skuli hiyo siku kiongozi huyo alipotembelea vijiji vya Bweleo na Fumba kukagua miradi ya maendeleo na chanagamotozinazowakabili wananchi wa vijiji hivyo.
Mmiliki wa eneo lenye Magofu ya Bwefum, Bwana Chandra (wa kwanza kulia) akitoa maelezo kwaa Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi kufuatia mgogoro wa muda mrefu kati yake na Wananchi wa Kijiji Hicho. Balozi
Seif alizitaka pande hizo kuwa na subra wakati Serikali inafanya utafiti
utakaopelekea kupatikana kwa maamuzi sahihi ya kusuluhisha mgogoro huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya ujenzi wa Uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu wa kijiji cha
Bweleo, Hassan Gharib (wa pili kushoto) akitoa maelezo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi juu ya changamoto wanazoipambana
nazo katika kutimiza azma yao. Wa kwanza kulia alievaa miwani ni mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Zanzibar (BTMZ) Sharifa Khamis.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifurahia bidhaa
zilizotengenezwa na Kikundi cha Ushirika cha Ukweli ni Njia Safi cha Kijiji cha
Bweleo. Kikundi hicho kinazalisha bidhaa mbali mbali za matumizi ya urembo na kawaida kwa kutumia mwani na mazao mengine ya baharini hali iliyomshawishi makamo huyo wa Rais kununua baadhi ya bidhaa hizo.
Subscribe to:
Posts (Atom)